WOSIA
X. AGIZO LA KUMI
IMANI YA KUZISHIKA KANUNI TAKATIFU
"Anayeishi katika kanuni anaishi na Mungu".
Kwa kanuni tunaelewa: katiba yetu, sheria ambazo zinatuelewa tafsiri ya kiroho ya kanuni takatifu.
Kuwa mwaminifu katika kanuni takatifu ni maisha ya kunyoka na ya hakika. Hatuwezi kufikiri jambo bora zaidi.
Kanuni zetu ni hazina yetu, sababu ni kwetu sisi wonyesho wa wazi na wa uhakika ya mapenzi ya Mungu kwetu sisi na ndio maana zinapaswa kuwa kwetu na thamani isiyo na mwisho.
Hatuhitaji kuchoka kwa kuzitafuta, sisi tunazo na tunaishi nazo, zimetuzunguka kila hatua. Kama ndege angani na samaki majini, hivi na sisi tumezamishwa katika mapenzi ya Mungu, yaonyeshwayo katika kanuni zetu Takatifu.
Ina maana gani kusema kuunganika na Mungu? Ina maana gani kusema kuunganika na mapenzi yake. Ni nani ambaye kwa undani ameunganika kabisa na Mungu? Yule ambae katika kila hatua anayatimiza mapenzi ya Mungu na mapenzi yake ameyaunganisha kabisa na yake Mungu.
Katika huku kuunganika na mapenzi ya Mungu, inatuongoza kwa uhakika mkubwa kanuni zetu Takatifu, sababu zinatuonyesha ni wapi penye mapenzi ya Mungu na zinatuwezesha kuyatimiza kila wakati.
Tuzipende, tuzipende kwa moyo wote kanuni zetu Takatifu, tujitahidi kuzifuata kwa uaminifu mkubwa. Tuziingize ndani ya mioyo yetu, tuzitafakari. Zenyewe ndio nguvu zetu, furaha yetu, alama inayotuongoza njia ya mbinguni, mwanga wetu, maana zinaeleza wazi mapenzi ya Mungu.
Tusijiondoe katika ukamilifu mwaminifu wa kanuni Takatifu. Zenyewe zatuonya wakati mwingine, zinazuia tabia yetu mbovu ya asili, na hiyo ni nzuri hata kama tabia haipendi. Kanuni zinatusaidia kuondoka kwenye vifungo vya u "mimi" duniani na kutuinua juu, kuelekea kwa Mungu, kwa mabawa ya mapenzi yake.
Basi tuchukue juu yetu na kwa ushujaa na kwa kadiri nzuri, mzigo, Kanuni Takatifu. Huu mzigo ni kwa anayempenda Mungu, ni mwepesi na Mtamu, sababu ni mapenzi ya Mungu, mema yasiyo na mwisho, matakatifu na yenye hekima. Ni hazina yetu, ni yote yetu duniani.